Kuna msichana
mmoja aliona maisha magumu mno, kila alichokifanya alikiona kushindikana jambo
lililomkatisha tamaa. Kila alipokuwa akilitatua
tatizo hili, kuna tatizo jingine liliinuka na kumfanya kuchanganyikiwa.
Hakutaka kuendelea
kuishi maisha ya namna hiyo, alichoamua kukifanya ni kumfuata mama yake na
kisha kumuelezea matatizo aliyokuwa akikutana nayo. Sauti yake tu, ilisikika
kama mtu aliyekuwa amekata tamaa na kutokata kuendelea na maisha yale.
Mama yake hakusema
kitu, alichokifanya ni kumchukua na kumpeleka jikoni. Akachukua maji na
kuyaweka jikoni, yalipocheka, akachukua karoti akaziingiza katika maji yale,
akachukua mayai na kuyaingiza katika maji yale na mwisho kuchukua kahawa na
kisha kuiingiza katika maji yale bila kusema kitu chochote kile.
Kila kitu
kilipochemka, akayatoa mayai yale na kisha kutoa karoti zile katika maji yale
na kisha kumuuliza 'UMEONA NINI?'
"Nimeona karoti, mayai na kahawa," alijibu.
"Nimeona karoti, mayai na kahawa," alijibu.
Mama yule akamtaka
binti yake aziguse karoti zile, binti alipozigusa, akagundua kwamba karoti
zimekuwa laini sana. Hakuishia hapo, akamtaka ayachukue mayai yale na
kuyavunja.
Yule binti alipoyavunja, akagundua kwamba yamekuwa magumu tofauti na kipindi kile, kabla ya kuyaingiza ndani ya maji yale yaliyokuwa yamechemka.
Yule binti alipoyavunja, akagundua kwamba yamekuwa magumu tofauti na kipindi kile, kabla ya kuyaingiza ndani ya maji yale yaliyokuwa yamechemka.
Mwanamke yule
hakuishia hapo, akamwambia aonje maji yale yaliyokuwa yamechanganywa kahawa,
alipoyaonja, akayahisi yamebadilika ladha na kuwa matamu sana.
"Una maana
gani kufanya haya yote mama?" msichana yule alimuuliza mama yake aliyeanza
kumjibu hivi:
"Kabla
sijaweka karoti ndani ya maji, zilikuwa ngumu sana ila baada ya kuziweka ndani
ya maji yanayochemka, zikabadilika na kuwa laini sana. Sikuishia hapo,
nilichokifanya ni kuyachukua mayai na kisha kuyaweka ndani ya maji
yanayochemka, kilichotokea, mayai yale yaliyokuwa laini, yakabadilika na kuwa
magumu.
"Nilipoweka
kahawa ndani ya maji, matokeo yake kahawa ile ikabadilisha maji yote. Kumbuka
kwamba vitu hivyo vitatu vimepitia katika kitu kimoja, maji yaliyokuwa
yakichemka. Hebu niambie binti yangu, wewe ni nani? Karoti, yai au
kahawa?"
CHA KUJIFUNZA
Wote tunapitia
katika matatizo mbalimbali. Hatutakiwi kuwa karoti kwamba tunapopitia humo
tunakuwa laini na mwisho kukata tamaa, wote tunatakiwa kuwa kama yai, tunaingia
humo kwenye matatizo tukiwa legevu lakini mara tunapoyashinda tunakomaa na kuwa
wenye nguvu na wagumu. Ila pamoja na hayo yote, katika kipindi ambacho
tunapitia katika matatizo mbalimbali yatupasa kuwa kahawa zaidi, kwa kupitia
matatizo yetu basi marafiki zetu wote wanaotuzunguka waweze kubadilika kupitia
sisi na hata wakati mwingine kuwabadilisha wale ambao wametufanya sisi kuingia
katika matatizo hayo.
HEBU KUWA MUWAZI,
UNAPOINGIA KWENYE MATATIZO WEWE HUWA NANI? KAHAWA, YAI AU KAROTI?

Maoni